ABDULKARIM SUMA





NEWS

  Libya yamhoji balozi wa Marekani kuhusu Liby



Majeshi ya Marekani yaliyomkamata Al Liby mjini Tripoli
Serikali ya Libya imemhoji balozi wa Marekani nchini humo kuhusu hatua ya majeshi ya Marekani kumkamata mshukiwa wa kundi la kigaidi la Al Qaeeda ndani ya nchi hiyo.
Anas al-Liby, alikuwa anasakwa kwa udi na uvumba tangu kuongoza mashambulizi ya kigaidi dhidi ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania mwaka 1998.
Anas al-Liby alikamatwa Jumamosi na wanajeshi wa Marekani mjini Tripoli.
Waziri mkuu wa Libya, Ali Zeidan alisema kuwa uhusiano kati ya Marekani na nchi hiyo hautaathirika kutokana na kukamatwa kwa al Liby nchini humo.
Bwana Zeidan alisema kuwa raia wa Libya lazima wahukumiwe nchini Libya. Waziri wa haki na sheria naye akasema kuwa anahitaji maelezo kuhusu swala hilo.
Marekani imesema kuwa mpango wake wa kumkamata al Liby ulikuwa halali
Mwanawe Liby, Abdullah al-Ruqai, amesema kuwa babake alikamatwa na watu waliokuwa wamejifunika nyuso zao na kuwa baadhi yao walikuwa raia wa Libya.
Anaamini kuwa serikali ya Libya pia ilihusika na kutoweka kwa babake, madai ambayo Libya imeyakanusha vikali.
Waziri wa sheria wa Libya Salah al-Marghani alitaka kikao na balozi wa Marekani kujadili swala hilo, Jumatatu asubuhi wakati maandamano yakifanyika mjini Benghazi kuhusu kukamatwa kwa Anas al-Liby.
Naye balozi wa Marekani aliambia BBC kuwa alikuwa katika mazungumzo na serikali ya Libya ikiwemo wizara ya mambo ya nje ya nchi hiyo.
Bwana Marghani na maafisa wengine kutoka katika wizara ya mambo ya nje pia walikutana na familia ya Liby waliofahamishwa kuhusu mazungumzo yao na balozi wa Marekani.
Liby – ambaye jina lake la kweli ni Nazih Abdul-Hamed al-Ruqai – anaaminika kuwa mmoja wa wale walioongoza mashambulizi dhidi ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania na kusababisha vifo vya watu 220 .
Liby ameshitakiwa nchini Marekani kuhusiana na mashambulizi hayo na amekuwa kwenye orodha ya watu wanaosakwa sana na shirika la ujasusi la FBI kwa zaidi ya miaka kumi huku mwenye taarifa kumhusu akiahidiwa zawadi ya dola milioni 5.
Marekani imetetea hatua yake ya kumkamata al Liby ikisema kuwa walifanya hivyo kwa kuzingatia sheria na kuwa atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka dhidi yake.

 

ICC yamruhusu William Ruto kurejea Kenya

Majaji katika mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC wameahirisha kesi ya naibu Rais wa kenya William Ruto kwa juma moja ili kumpa mda kurejea nyumbani kushughulikia hali ya kiusalama inayokumba taifa hilo.
Watu wanoaminika kuwa magaidi wa Al Shabaab wameteka jumba la kifahari lenya maduka la Westgate jijini Nairobi na kuwazuilia mateka wakenya kadhaa.
Bwana Ruto anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kibinadamu kufuatia ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007 nchini kenya.
Ruto na Rais Uhuru Kenyatta, wanakabiliwa na tuhuma za za uhalifu dhidi ya binadamu baada ya kudaiwa kuhusika na ghasia za kikabila baada ya uchaguzi wa mwaka 2007-2008 ambapo watu zaidi ya elfu moja waliuawa.
Mahakama iliakhirisha kesi baada ya kikao cha dharura kuitishwa huku upande wa mashtaka ukisema kuwa hauna pingamizi lolote ikiwa kesi zitaakhirishwa kwa muda mfupi.
Mwakilishi mmoja wa mashahidi aliangua kilio mahakamani na kutaka mahakama iweze kumruhusu Ruto kurejea nyumbani kushughulikia swala hilo la dharura.
''Kutokana na hali ilivyo na maoni tuliyoyasikia , mahakama inamruhusu Ruto kurejea nyumbani kwa muda wa wiki moja,'' alisema jaji anayesimamia kesi hiyo, Chile Eboe-Osuji.
"Kwa sasa Ruto ataruhusiwa kusalia Kenya kwa wiki moja, ila ikiwa atatoa ombi lengine,'' alisema jaji Chile.
Kwa mujibu wa wakili wa Ruto,Karim Khan, alitarajiwa kuondoka Uholanzi saa tatu asubuhi, saa za Afrika Mashariki

 

Vikosi vya usalama vyaingia Westgate

Milio mikubwa ya risasi na milipuko imesikika huku juhudi za usalama zikiendelea katika jengo la Westgate ambako wanamgmbo wa Al shabaab wameteka jengo hilo pamoja na wakenya wachache ambao wangali kuokolewa.
Kwa mujibu wa waziri wa usalamaJoseph Ole Lenku, vikosi vya usalama vimeweza kudhibiti jengo hilo kutoka nje na ndani na kwamba ni mateka wachache walosalia katika jengo hilo.
Serikali inasema watu 62 wameuawa lakini shirika la Red Cross lilisema kuwa idadi hiyo ni 69.
Westgate ni jumba la kifahari lenye maduka na mikahawa karibia themanini .
Milio hiyo ilidumu kwa dakika tatu na kufuatiwa na moshi mkubwa juu ya jengo hilo. Hakuna taarifa kamili kuhusu kilichosababisha moshi huo.
Wapiganaji wa Al shabaab wamewateka nyara raia ambao idadi yao haijulikani. Walikuwemo ndani ya jengo wakiendelea na shughuli zao kuanzia Jumamosi mchana wakati wapiganaji wa Al shabaab walipowavamia na kuanza kufyatua risasi kiholela.
Inaarifiwa kuna maiti kumi katika ghorofa ya kwanza ya jengo hilo.
Aidha wapiganaji hao wanaoaminika kuwa wanachama wa Al Shabaab ni kati ya kumi na kumi na watano na bado wangali ndani ya jengo hilo.
Ripoti zinasema kuwa ufyatulianaji mkubwa wa risasi pamoja na milipuko imesikika katika jengo hilo kwa takriban dakika 15.
Harakati za kuendelea kumaliza operesheni hiyo zinaendelea lakini hali ya mateka walio ndani ya jengo hilo inaendelea kudorora.

Wakenya waliofanikiwa kuondoka katika jengo la Westgate kwa usaidizi wa polisi
Rais Kenyatta amesema kuwa jeshi linajitahidi kuhakikisha kuwa linakabiliana vilivyo na wanamgambo hao.
Helikopta za polisi zinazunguka juu ya jengo hilo pamoja na ndege za kijeshi kushika doria. Vikosi vya usalama vinaendelea na operesheni kujaribu kuwanusuru waathiriwa wakati hali ikiwa ni ya ati ati katika eneo la shambulizi.
Awali jeshi la Kenya lilisema limeweza kudhibiti jengo hilo lote ingawa bado limetaja hali kuwa tete mno hasa katika kujaribu kuwaokoa mateka waliosalia ndani ya jengo hilo.
Ripoti zinasema kuwa watu 69 wamefariki katika shambulizi hilo la Al Shabaab kufikia sasa huku 175 wakijeruhiwa. Baadhi wametibiwa na kuondoka hospitalini. Baadhi ya majeraha waliyopata ni majereha ya risasi na kutokana na guruneti ambalo Al shabaab waliwarushia wale waliokuwa ndani ya mikahawa siku ya Jumamosi.
Kundi hilo limekiri kutekeleza shambulio hilo kutokana na hatua ya Kenya kupeleka majeshi yake nchini Somalia ili kukabiliana na wapiganaji hao.

Matukio ya hivi punde Westgate



Vikosi vya usalama vinaendelea na juhudi za kukabiliana na magaidi walioteka nyara baadhi ya wakenya huku mateka wakinusuriwa
Unahitaji toleo sahihi la Flash Player kucheza sauti/video
Vikosi vya usalama vinaendelea na juhudi za kukabiliana na magaidi walioteka nyara baadhi ya wakenya katika jengo la Westgate
Katika ukurasa huu tutakupasha moja kwa moja matukio yanavyojiri katika jengo la Westgate.
Ikiwa uko karibu na jengo hilo unaweza kutupasha hali unavyoiona kupitia kwa ukurasa wetu wa Bofya facebook bbcswahili

Bofya Facebook: Halima Msuya kutoka Moshi kupitia Bofya bbcswahili Ameandika Poleni sana ndugu zetu Mungu yu pamoja nanyi.
Bofya Facebook: Mohamed Kahogo Wa Morogorogo Tzn asema kwenye ukrasa wa Bofya bbcswahili Eee Mola wajaalie hawa ndugu zetu wakenya!waushide mtihani huu AMEEEN.
15:33 Waziri wa usalama wa Kenya Joseph Ole Lenku asema kuwa wanajeshi wameweza kudhibiti jengo lote la Westgate
15:20 Polisi waonekana wakikimbia huku na kule katika harakati zao hizo dhidi ya Al Shabaab



Juhudi za uokozi Westgate
14:56 Mkuu wa majeshi Meja Jenerali Julius Karangi amesema magaidi hao wanaweza kujisalimisha ikiwa wanataka kwa sababu jeshi litakabiliana nao vilivyo. Pia amesema kuwa Kenya inakabiliana na magaidi wa kimataifa

14:35 Ole Lenku anasema kuwa hali ingali tete lakini vikosi vya usalama vya Kenya vinakaribia kuwazingira magaidi hao...Hadi kufika sasa watu 62 wamefariki na wengine zaidi ya 175 kujeruhiwa. Pia ameongeza kuwa magaiodi wote ni wanaume, kutokana na taarifa za awali kuwa magaidi hao walikuwa wanaongozwa na mwanamke

14:30 Ole Lenku anasema kuwa wanajeshi kumi wamejeruhiwa na wanapokea matibabu. Pia mateka karibu wote wameweza kuokolewa. Ole Lenku pia amesema kuwa wameweza kuwaua magaidi wawili

14:28 Waziri wa usalama Joseph Ole Lenku anasema kuwa moshi ulitokana na moto uliosababishwa na magaidi wlaioko ndani ya jengo hilo kujaribu kusambaratisha juhudi za wanajeshi wa Kenya dhidi yao



Moshi mkubwa ukitoka ndani ya jumba la Westgate
14:03 Mkuu wa polisi David Kimaiyo asema kuwa vikosi vya usalama vinakaribia kudhibiti jengo hilo lote na vimeingia ndani kabisa ya jengo hilo kiasi cha kuwaokoa baadhi ya mateka
14:00 PM: Milipuko zaidi yasikika katika jengo hilo

13:54: Mwandishi wa BBCIdriss Situmaaliye katika eneo la Westgate anasema duru zinaarifu kuwa vikosi vya usalama vya Kenya vinasema kuwa ndivyo vimelipua sehemu ya jengo kujaribu kuingia ndani kabisa ya jengo hilo
13:52 PM Magari ya Ambulance yaobnekana yakienda katika eneo la shambulizi pamoja na magari ya zima moto. Vikosi vya usalama vinawataka watu kuondoka karibu na eneo la operesheni hiyo ili kuwawezesha kufanya kazi yao



Waathiriwa wa shambulizi la Westgate
13:49 pm: Moshi mkubwa mweusi waonekana ukitoka juu ka juu katika jengo hilo haijulikani nini kilichosababisha
13:19 pm Moshi mkubwa unaonekana ukitoka katika jengo la Westgate ambako wapiganaji wa Al Shabaab wanawazuilia mateka wakenya ambao idadi yao haijulikani

13:12 PM Viongozi wa kidini watoa taarifa kulaana kitendo cha Al Shabaab
12:30 PM: Milipuko zaidi na milio ya risasi imesikika katika jengo la Westgate huku vikosi vya usalama vikifanya jitahada za misho kuwa

 

 

 

Al shabaab ni nani hasa?



Wapiganaji wa Al Shabaab
Kundi la wapiganaji wa kisomali la al-Shabaab,limevamia jumba la kifahari lenye maduka na mikahawa nchini Kenya. Al Shabaab lenya mizizi yake nchini Somalia, limeweza kuondolewa kutoka miji mikubwa ya Somalia ikiwemo Mogadishu na sehemu zengine za Somalia , ingawa bado linasalia kuwa tisho kubwa kwa kanda nzima.

Al Shabaab ni nani?

Jina Al-Shabab linamaanisha Kijana kwa lugha ya kiarabu. Kundi hilo liliibuka kama tawi la vijana la muungano wa mahakama za kiislmau ambao baadaye ulivunjika mwaka 2006, wakati ilipopigana na wanajeshi wa Ethiopia waliokuwa wameingia nchini Somalia kuunga mkono serikali iliyokuwa dhaifu.
Kuna taarifa chungu nzima kuhusu wapiganaji wa kiisilamu wanaokwenda Somalia kupigania Al Shabaab.
Kundi hilo limeweka sheria kali za kiisilamu katika maeneo ambayo linadhibiti ikiwemo kupigwa kwa mawe hadi kufa wanawake wanaodaiwa kufanya uasherati pamoja na kuwakata wezi mikono.

Je Al Shabaab linadhibiti sehemu gani ya Somalia?

Ingawa kundi hilo limepoteza udhibiti, wa miji mikubwa, bado linakita mizizi katika maeneo ya mashinani.
Lililazimika kuondoka katika mji mkuu Mogadishu, mwezi Agosti mwaka 2011 na pia kuondoka katika mji wa bandarini wa Kismayo mwezi Septemba mwaka 2012.
Kismayo ulikuwa mji muhimu kwa kundi hilo, ambao ulikuwa unawezesha bidhaa kuwafikia wapiganaji wa kundi hilo pamoja na kuwatoza watu ushuru kwa shughuli zao.

Hizi ni silaha za Al Shabaab walizonasa wanajeshi wa AU
Muungano wa Afrika, ambao unaunga mkono juhudi za majeshi ya serikali, ulisherehekea ushindi huo ingawa al-Shabab hunfanya mashambulizi ya mara kwa mara ya kujitoa mhanga mjini Mogadishu na kwingineko.
Wadadisi wanaamini kuwa al-Shabab limeanza kufanya mashambulizi ya kuvizia baada ya kushindwa na majeshi ya Muungano wa Afrika wanaotumia nguvu dhidi yao.
Lakini linakabiliwa na tisho kubwa kutoka kwa wanajeshi wa Kenya walianza hatarakti zao dhidi ya kundi hilo kuanzia mwaka 2011.
Kenya ilituhumu wapiganaji wa al-Shabab kwa kuwateka nyara wanajeshi wake pamoja na watalii na sasa wamekuwa katika msitari wa mbele kupambana na kundi hilo la kigaidi.
Wakati huo, wanajeshi wa Ethiopia waliweza kukabiliana na wapiganaji hao na kudhibiti miji ya Beledweyne na Baidoa.

Nani kiongozi wa al-Shabab?

Ahmed Abdi Godane ndiye kiongozi wa kundi hilo. Anajulikana kama Mukhtar Abu Zubair, na anatoka katika jimbo la Somaliland.
Kumekuwa na taarifa za mgawanyiko katika kundi hilo, ambazo hata hivyo zinapingwa vikali na kundi lenyewe. Inaarifiwa kuwa uongozi wake unapingwa, na wanachama wanaotoka maeneo ya Kusini na ambao ni wengi katika kundi hilo. Inakisiwa idadi yao ni kati ya wanajeshi 7,000 na 9,000.
Bwana Godane huwa haonekani hadharani . Mtangulizi wake Moalim Aden Hashi Ayro, aliuawa katika shambulizi lililofanywa na Marekani mwaka 2008.

Nini uhusiano wa kimataifa wa kundi hilo?


Al Shabaab wakifanya mashambulizi mjini Mogadishu
Al-Shabab lilijiunga na al-Qaeda mwezi Februari mwaka 2012. Katika ujumbe wa Video, kiongozi wa al-Shabab Ahmed Abdi Godane alisema anaahidi kuunga mkono kingozi wa al-Qaeda Ayman al-Zawahiri.
Makundi hayo mawili yamekuwa yakifanya kazi kwa pamoja, na raia wa kigeni wamekuwa wakiunga mkono kundi hilo, na hata kuwasaidia katika harakati zao za mapigano.
Mwaka jana maafisa wa al-Shabab waliambatana na mtu aliyesema ni mwanachama wa al-Qaeda na kumtambua kuwa raia wa Marekani Abu Abdulla Almuhajir alipokuwa anatoa msaada wa chakula kwa waathiriwa wa njaa.
Maafisa nchini Marekani wanaamini kuwa wapiganaji wa Al Qaeeda ambao hawajahusina sana na mashambulizi nchini Afghanistan na Pakistan kufuatia mauaji ya kiongozi wao,Osama bin Laden, wapiganaji wake wengi wanakwenda kutafuta hifadhi nchini Somalia.

 

 

30 wauawa na magaidi Nairobi, Kenya


Majeruhi katka kisa cha uvamizi wa duka la ghorfa nne Nairobi. 

Kufuatia watu wenye silaha kuvamia jengo la ghorofa nne lenye maduka la Westgate jijini Nairobi sasa inahofiwa angalu watu 30 wameuawa na wengine zaidi ya hamsini kujeruhiwa vibaya.
Kwa mujibu wa taarifa za Shirika la Msalaba mwekunde la Kenya idadi ya waliofariki imeongezeka hadi 30. Washambulizi wangali ndani ya jengo hilo na inaaminika wangali wamewateka nyara baadhi ya watu waliokuwa katika duka hilo.
Wakati huo huo taarifa kutoka ikulu ya Rais Kenya inasema kwamba serikali imeanzisha oparesheni kali ya uokozi.
Hii nikutokana na taarifa kwamba watu hao wenye silaha wanawashikilia mateka watu kadhaa ndani ya jengo hilo.
Mtu mmoja ambaye amejificha ndani ya jengo hilo ameiambia BBC kwamba ameona watu wapatao 36 wakiwa wameshikwa mateka na waru hao.
Hata hivyo Ikulu ya Kenya imesema ni mapema sana kusema kwamba tukio hilo ni la kigaidi.
Ikulu ya Nairobi vilevile imesema ni mapema mno kusema kama uvamizi huo ni tukio la kigaidi au la.
Walioshuhudia kisa hicho wanasema watu waliovalia magwanda yalioonekana kama ya kijeshi huku wengine wakiwa wamefunika nyuso zao walivamia jengo hilo kwa wakifyatua risasi.
Kisa hicho kimetokea katika eneo la kifahari la Westland jijini Nairobi .


Jengo la Duka lililovamia wa watu wenye silaha

Maduka hayo ya Westgate hupendelewa sana na watu matajiri na wageni.
Walioshuhudia tukio hilo, wanasema kuwa maguruneti piya yalitumika.
Polisi waliojihami kwa silaha wamezingira jengo la maduka liitwalo Westgate, katika mtaa wa Westlands, na kuna taarifa ya watu waliojeruhiwa wakitolewa hapo kwa machera.
Hadi sasa kuna watu ambao idadi yao haijulikani wamo ndani ya jengo hilo.
Wakati huo huo Hospitali ya Aga Khan, ya Nairobi imetoa ujumbe wa dharura kwamba damu inatakikana kwa haraka.
Hii ni kutokana na taarifa kwamba kuna idadi kubwa ya majeruhi ambao wamepelekwa katka hospitali hiyo.

 

Al shabaab: ''Kenya ilipuuza onyo letu''



Duka la kifahari lililoshambuliwa la Westgate katika mtaa wa Westlands Nairobi

Afisaa mmoja mkuu wa kundi la kigaidi la Alshabaab, amefahamisha BBC kuwa kundi hilo ndilo limehusika na shambulizi dhidi ya duka la kifahari la Westage mjini Nairobi Kenya.
Kwa mujibu wa Afisaa huyo mashambulizi hayo yalikuwa ya kulipiza kisasi kwa Kenya kwa kujihusisha na vita vya Somalia ambako wanajeshi wake wanakabiliana na kundi hilo.
Wanajeshi wa Kenya wamekuwa nchini humo tangu mwaka 2011 kama sehemu ya juhudi za muungano wa Afrika kutaka kurejesha uthabiti nchini Somalia.
Afisaa mkuu wa mambo ya ndani Kenya amesema idadi ya waliofariki ni kumi na moja lakini shirika la msalaba mwekundu linasema idadi hiyo imefika watu 30 huku zaidi ya hamsini wakijeruhiwa.
Taarifa kutoka Ikulu ya Rais Kenya zinasema kuwa mshukiwa mmoja aliyekamatwa alifariki kutokana na majeraha yake.


 Baadhi ya watu waliofanikiwa kukimbilia usalama wao

Wanamgambo wa Al Shabaab kupitia kwa mtandao wao wa Twitter , wanasema kuwa Kenya haikuchukulia kwa uzito onyo walilotoa kwa taifa hilo kwa hatua ya kuwapeleka wanajeshi wake nchini humo kupambana dhidi yao.
Kundi hilo limesema limekuwa likitoa onyo mara kwa mara kwa Kenya kuwa ikiwa haitaondoa vikosi vyake nchini Somalia, athari zitakuwa mbaya mno.
Kupitia mtandao wao wa Twitter, Al Shabaab limesema kuwa Kenya ilijidai kutosikia onyo hizo, na kuendelea kuwaua waisilamu wasio na hatia nchini Somalia.
Taarifa hiyo ya Twitter ilisema kuwa Shambulio la Westgate ni tone tu katika bahari ya mfano wa yanayowakumba wasomali nchini Somalia.
Taharuki ilianza hii leo saa saba mchana wakati watu wanaokisiwa kuwa kumi walipovamia jengo la kifahari la Westgate la kuwapiga risasi kiholela wakenya waliokuwa wanaendelea na shughuli zao za kawaida.
Kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu , takriban watu 30 walifariki kwa kupigwa risasi au kutokana na majeraha yao na wengine wengi wenye majeraha ya risasi kukimbizwa hospitalini kwa matibabu.

 

 

"Magaidi" wauwa watu zaidi ya 20 Nairobi




Majeruhi katka kisa cha uvamizi wa duka la ghorfa nne Nairobi.
Kufuatia watu wenye silaha kuvamia jengo la ghorofa nne lenye maduka la Westgate jijini Nairobi sasa inahofiwa watu zaidi ya 20 wameuwawa kwa kupigwa riasasi.
Shirika la Msalaba mwekunde la Kenya limetoa taarifa likisema watu waliouwawa kwa kupigwa risasi ni 22.
Wakati huo huo taarifa kutoka ikulu ya Kenya inasema kwamba serikali imeanzisha oparesheni kali ya uokozi.
Hii nikutokana na taarifa kwamba watu hao wenye silaha wanawashikilia mateka watu kadhaa ndani ya jengo hilo.
Mtu mmoja ambaye amejificha ndani ya jengo hilo ameiambia BBC kwamba ameona watu wapatao 36 wakiwa wameshikwa mateka na waru hao.
Hata hivyo Ikulu ya Kenya imesema ni mapema sana kusema kwamba tukio hilo ni la kigaidi.
Ikulu ya Nairobi vilevile imesema ni mapema mno kusema kama uvamizi huo ni tukio la kigaidi au la.
Walioshuhudia kisa hicho wanasema watu waliovalia magwanda yalioonekana kama ya kijeshi huku wengine wakiwa wamefunika nyuso zao walivamia jengo hilo kwa wakifyatua risasi.
Kisa hicho kimetokea katika eneo la kifahari la Westland jijini Nairobi
.

 Jengo la Duka lililovamia wa watu wenye silaha

Maduka hayo ya Westgate hupendelewa sana na watu matajiri na wageni.
Walioshuhudia tukio hilo, wanasema kuwa maguruneti piya yalitumika.
Polisi waliojihami kwa silaha wamezingira jengo la maduka liitwalo Westgate, katika mtaa wa Westlands, na kuna taarifa ya watu waliojeruhiwa wakitolewa hapo kwa machera.
Hadi sasa kuna watu ambao idadi yao haijulikani wamo ndani ya jengo hilo.
Wakati huo huo Hospitali ya Aga Khan, ya Nairobi imetoa ujumbe wa dharura kwamba damu inatakikana kwa haraka.
Hii ni kutokana na taarifa kwamba kuna idadi kubwa ya majeruhi ambao wamepelekwa katka hospitali hiyo.

 

 

 

44 WAUAWA KINYAMA MSIKITINI, NIGERIA


Mauaji hayo yalifanyika wakati wa maombi ya asubuhi Jumapili , ingawa taarifa zimejitokeza Jumatatu , kutokana na hitilafu ya mawasiliano kwani jimbo hilo liko chini ya sheria ya hali ya hatari.
                             Maiduguri ni moja ya majimbo yaliyowekewa sheria ya hali ya hatari
Washambulizi wanasemekana kuwa wanachama wa kundi la wapiganaji la Boko Haram, ambalo liliwaua maelfu ya watu tangu mwaka 2009.Shambulizi lilifanyika katika mji wa Konduga, ulio umbali wa kilomita 35 kutoka mji mkuu wa jimbo hilo , Maiduguri.
Gazeti la Daily Post, liliripoti kuwa watu wengine 26 walikuwa wanatibiwa kwa majeraha waliyopata wakati wa shambulizi hilo hospitalini Maiduguri.
Mwanachama wa kikundi cha vijana kinachotoa ulinzi kwa raia, aliambia shirika la habari la Associated Press, kuwa wapiganaji wao wannne waliuawa walipojaribu kutoa kilio cha kutaka usaidizi.
Raia wengine kumi na wawili, waliuawa katika kijiji cha Ngom kinachopakana na Maiduguri.
Rais Goodluck Jonathan alitangaza sheria ya hali ya hatari katika majimbo matatu Kaskazini Mashariki mwa nchi mnamo mwezi Mei wakati wanajeshi walipofanya operesheni dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu.
Boko Haram linapigania eneo la Kaskazini mwa nchi likitaka kujitawala kwa kutumia sheria za kiisilamu.
Mwandishi wa BBC mjini Lagos, anasema kuwa wakati kundi hilo limekuwa likishambulia makanisa, pia limekuwa likishambulia misikiti.
Habari za mashambulizi hayo zilijitokeza wakati kanda ya video ya kiongozi wa kundi hilo Abubakar Shekau, ilipotolewa akidai kundi hilo kuhusika na mashambulizi hayo ikiwemo kushambulizi dhidi ya vituo vya polisi na kambi za jeshi.

Obama aahidi Kenya msaada kuhusu JKIA



Ndege za kimataifa zimeanza kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa jijini Nairobi JKIA, siku moja tu baada ya kitengo cha kuwasili wageni kuchomwa na moto mkubwa.
Ndege ya kwanza ya kimataifa kuwasili katika uwanja huo ni ile iliotoka Uingereza na baadaye nyengine kutoka Tanzania na Bangkok zikawasili.
Wachunguzi hata hivyo wanatafuta mabaki ya moto huo ili kutathmini chanzo chake.
Wakati huo huo Rais wa Marekani, Barack Obama amesema ataisaidia serikali ya Kenya katika kukarabati uwanja huo wa ndege baada ya moto mkubwa kuuteketeza hapo jana.
Katika ujumbe wake wa simu, Obama alisisitiza kuwa Marekani iko tayari kuisadia Kenya katika hali ile yoyote kutokana na ushikiano wake na Kenya.
Obama pia aliwapa pole familia zilizowapoteza wapendwa wao katika mashambulizi ya bomu ya Agosti 1998 mjini Nairobi.
Manmo Jumatano, moto mkubwa uliotokea majira ya asubuhi, uliharibu kitengo cha kuwasilia wageni wa kimataifa.
Vikundi vya wachunguzi viliwasili katika uwanja huo kufanya uchunguzi wao kubaini kilichosababisha moto huo.
Abiria walikwama kutokana na mkasa huo ingawa waliweza kuondolewa nje ya uwanja kwa ajili ya usalama wao huku baadhi wakiangalia mizigo yao ikiteketea wasijue la kufanya. .
Rais Uhuru Kenyatta aliwasili katika uwanja huo na kujionea uharibifu uliotokea na kiisha kutoa taarifa yake kupitia kwa msemaji wake Esipisu aliyesema kuwa chanzo cha moto huo kinachunguzwa.

Maandamano yafanyika nchini Tunisia

 26 Julai, 2013 - Saa 12:03 GMT

Mohamed Brahmi
Tunisia inashuhudia mgomo wa taifa zima baada ya kuuawa kwa kiongozi wa upinzani Mohamed Brahmi.
Chama cha wafanyakazi kikubwa kuliko vyote nchini Tunisia, UGTT, kimetoa wito wa kuwataka wananchi kupinga "ugaidi, ghasia na mauaji".
Alhamisi polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji katika miji kadhaa nchini humo, baada ya Bwana Brahmi kuuawa kwa kupigwa risasi nje ya nyumba yake mjini Tunis.
Chama tawala nchini Tunisia, cha Kiislam cha Ennahda kimekanusha tuhuma kutoka kwa ndugu wa marehemu kuwa kilikula njama katika mauaji ya Bwana Brahmi.
Yameelezea hofu kuhusu operesheni ya kijeshi inayopangwa na Umoja wa Mataifa yakisema itavuruga zaidi hali ya kibinadamu

 

 

Marekani kuchelewesha ndege kwa Misri

 25 Julai, 2013 - Saa 07:49 GMT

Marekani inanuia kuikabidhi Misri ndege 20 za kivita
Marekani imesema kuwa itachelewesha mpango wake wa kuikabidhi Misri ndege za kivita aina ya F-16 huku mgogoro wa kisiasa ukiendelea kutokota nchini Misri kufuatia kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa Rais Mohammed Morsi.
Msemaji wa idara ya ulinzi nchini Marekani, George Little alisema kuwa uamuzi huo ulifikiwa kutokana na hali inayokabili Misri kwa sasa.
Marekani inadadisi ikiwa kuondolewa mamlakani kwa Morsi ilikuwa mapinduzi ya kijeshi, hali inayoweza kusababisha Marekani kusitisha msaada wake kwa Misri.
Hapo jana mkuu wa jeshi la Misri Generali Sisi , aliitisha maandamano ya umma akiwataka wananchi kuliruhusu jeshi kukabiliana na kile alichokiita tisho la ugaidi.
Lakini Abdel Fattah al-Sisi aliongeza kuwa hakuwa anaitisha maandamano kwa lengo la vurugu huku akiwasihi wananchi kuwa na maridhiano.
Katika jibu lake kwa wito wa jeshi, chama cha Muslim Brotherhood, ambacho kinamuunga mkono Morsi, kilisema kuwa Generali Sisi alikuwa anaitisha vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Ndege hizo nne aina ya F-16 ni sehemu ya ndege nyingine 20 ambazo zimeitishwa, kati ya hizo nane tayari zikiwa zimepelekwa Misri.
Hata hivyo Marekani iliahidi tarehe 11 mwezi Julai kuwa bado ina mpango wa kuikabidhi Misri ndege hizo.

Papa apinga madawa ya kulevya

 25 Julai, 2013 - Saa 10:32 GMT

Baba mtakatifu akiwa katika ziara yake nchini Brazil
Kiongozi wa kanisa katoliki, Baba mtakatifu Francis, amekosoa vikali mipango ya kutaka kuhalalisha madawa ya kulevya Amerika ya Kusini.
Aliyasema hayo wakati alipotembelea klikini mpya ya kuwatibu waraibu wa dawa za kulevya mjini Rio de Janeiro.
Vyanzo vya matumizi mabaya ya madawa ya kulevya lazima vitatuliwe, alisema papa katika siku ya tatu ya ziara yake nchini Brazil.
Uruguay inakaribia kuidhinisha uuzaji wa Marijuana au Bhangi huku baadhi ya nchi katika kanda hiyo zikitafakari hatua sawa na hiyo.
Awali Papa Francis mzaliwa wa Argentina alishiriki misa yake ya kwanza katika ziara yake katika kanisa la Our Lady of Aparecida.
Aliwaonya maelfu ya waumini dhidi ya kukumbatia sana pesa, mamlaka na raha za dunia.
Baada ya ziara yake eneo la Aparecida, nchini Brazil Papa alirejea mjini Rio de Janeiro.
Wakati wa ufunguzi wa kliniki ya kutoa matibabu kwa waraibu wa madawa ya kulevya, aliwakumbatia waliokuwa watumizi wa dawa hizo, huku akiwasikiliza wakisimulia yaliyowakumba wakati wa uraibu wao.
"ni muhimu kukabiliana na vyanzo vya matumizi mabaya ya madawa ya kulevya, kuhakikisha haki na kuwafunza vijana kuhusu umuhimu maadili mazuri katika jamii, kuwasaidia wanaokabiliwa na matatizo na kuwapa matumaini,'' alisema Papa.
Papa Francis pia alionya dhidi ya mipango ya kuhalalisha madawa ya kulevya katika kanda ya Amerika ya Kusini huku akiwalaani walanguzi wa madawa hayo.
 
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete aongoza maelfu ya watanzania katika zoezi la kuaga miili ya wanajeshi saba waliofariki katika shambulizi la ghafla huko Darfur, baadaye wanajeshi hao watasafirishwa kwenda kwao kwaajili ya mazishi.

 

 

9 wauawa kwenye ghasia nchini Misri

 23 Julai, 2013 - Saa 10:24 GMT
Watu tisa wameuawa mjini Cairo, Misri katika makabiliano yaliyodumu usiku kucha kati ya wafuasi na wapinzani wa rais aliyengo'lewa mamlakani Mohammed Morsi.
Maafisa wanasema kuwa , ghasia zilitokea wakati wa maandamano yaliyofanywa na wafuasi wa Morsi.
Familia ya Bwana Morsi imetuhumu jeshi kwa kumteka nyara kiongozi huyo wa zamani.
Rais huyo wa zamani amezuiliwa na jeshi katika sehemu isiyojulikana bila ya kufunguliwa mashtaka yoyote, tangu mkuu wa majeshi Generali Abdul Fattah al-Sisi, kutangaza kung'olewa mamlakani kwa Morsi tarehe 3 Julai.
Chama cha Bwana Morsi cha Muslim Brotherhood kimekataa kutambua serikali ya kijeshi huku kikifanya maandamano karibu kila siku kote nchini Misri.
Ghasia hizo zimesababisha vifo vya zaidi ya watu 60 tangu kuondolewa mamlakani kwa Morsi.
Siku ya Jumatatu mtu mmoja alifariki na wengine wengi wakijeruhiwa wakati wa maandamano mjini Cairo, kwa mujibu wa maafisa wa afya.
Televisheni ya taifa iliripoti kuwa wafuasi wa Morsi waliokuwa wanaandamana walikamatwa kwa umiliki haramu wa silaha.
Vifo zaidi vimeripotiwa katika makabiliano mengine tofauti katika mkoa wa Qalyubiya Kaskazini mwa Cairo.
Wakati huohuo, familia ya Morsi ilisema hawajawasiliana kamwe na Morsi, na ikathibitisha kuwa wanaitaka mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita kuanzisha uchunguzi juu ya kupinduliwa kwake.
Nchi kadhaa ikiwemo Marekani zimetaka Morsi aachiliwe.
Lakini maafisa wa kijeshi wanasisitiza kuwa anazuiliwa katika eneo

 

 

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema Akutana na Naibu Kamishina wa UNAMID Dkt. Syed Kaleem Imam, kutoka nchini Sudan, jimbo la Darfur


Rate This

 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema, akimkabidhi zawadi yenye nembo ya Jeshi Polisi Tanzania, Naibu Kamishina wa UNAMID Dkt. Syed Kaleem Imam, kutoka nchini Sudan, jimbo la Darfur, alipomtembelea ofisini kwake Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Dar es salaam, akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku sita hapa nchini.
Naibu Kamishina wa UNAMID Dkt. Syed Kaleem Imam, kutoka nchini Sudan, jimbo la Darfur (wapili kutoka kulia), akitoa mada katika kikao cha kubadilishana uzoefu kilichowashirikisha makamishina na maofisa waandamizi wa Jeshi la Polisi Nchini. Kutoka kulia ni Kamishina wa utawala na fedha wa jeshi la polisi, CP Clodwig Mtweve, Kamishina wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, CP Paul Chagonja, Mkuu wa tathmini na ufuatiliaji Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) Omar Rashid pamoja na Mkuu wa Utawala na rasilimali wa jeshi la Polisi (DCP)Thobias Andengenye.
Picha na Demetrius Njimbwi, Jeshi la Polisi Dar es Salaam 

WANAJESHI WA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA(JWTZ)WALIOUWAWA DAFUR KATIKA SHAMBULIO WAAAGWA,KUREJESHWA NCHINI


Rate This




  Mojawap0 ya magari ya askari hao likiwa limeharibika vibaya kutokana na shambulio hilo.
 Miili ya wanajeshi saba wa JWTZ waliouawa katika machafuko nchini Sudani, Darfur.  Askari hao walifariki wakiwa kwenye vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa huko nchini humo.  Majina yao ni (1)Sajenti Shaibu Othuman, (2)Koplo Oswald Chaula, (3)Koplo Mohamed Juma, (4)Koplo Mohamed Chikilizo, (5)Pte. Rodney Ndunguru, (6)Pte. Peter Werema na (7)Pte. Fortunatus Msofe
Al-Shabaab ayaa 18-kii Maajo sii daysay warqad furan oo ay soo marsiisay barteeda Tuwiterka taa oo ku tiimbareeynaysay "qas-wadayaasha diinteena" -- oo ah kalmad loo isticmaalay in lagu qeexo hoggaamiyayaasha sare ee al-Shabaab ee ka soo horjeeda hoggaamiyaha sare Axmed Cabdi Godane -- laguna tilmaayay "fulayo" isku dayaya in ay marin-habaabiyaan xubnaha hoose ee ururka iyagoo shaki galinaya hoggaamintiisa.
  • Sawir oo filayo in uu yahay kii ugu dambeeyay ee dagaalyahaniniinta al-Shabaab oo kasoo muuqday Tuwiterka rasmiga ah ee ururka bishii Abriil 30-keedii. [Keyd] Sawir oo filayo in uu yahay kii ugu dambeeyay ee dagaalyahaniniinta al-Shabaab oo kasoo muuqday Tuwiterka rasmiga ah ee ururka bishii Abriil 30-keedii. [Keyd]
  • Garabka warbaahinta al-Shabaab ee al-Kataib ayaa sii daayay warqadan ku taariikheeysnayd 18-kii Maajo iyagoo soo marsiiyay Tuwiterka rasmiga ah ee ururka. [Keyd] Garabka warbaahinta al-Shabaab ee al-Kataib ayaa sii daayay warqadan ku taariikheeysnayd 18-kii Maajo iyagoo soo marsiiyay Tuwiterka rasmiga ah ee ururka. [Keyd]
Warqadda, oo cinwaan looga dhigay "Muslimiinta oo Looga Digayo Khiyaanada Gaalada", ayaa waxaa qoray garabka warbaahinta al-Shabaab ee al-Kataib, oo iyaguna si lamid ah barta Tuwiterka, aalad borobogaando u ah Godane, oo inta badan loogu yeero Mukhtar Abu Subeyr.
"Waxaa nagasoo dhex baxay kuwa doonaya in ay kala dhantaalaan midnimada Muslimiinta guud ahaan iyo gaar ahaan Mujaahidiinta," ayaa warqadda lagu sheegay. "waxay doonayaan in ay weeraraan mujaahidiinta iyo hoggaamiyayaashooda oo ay shaki galiyaan tayadooda iyo qaab fikriyeedkooda. Waxa ay sidoo kale doonayaan in ay ruxaan kalsoonidooda iyo sido kale khidadahooda iyo siyaasadahooda iyagoo shaki galinaya Islaamnimadooda iyo Jihaadkooda."
Marka wax laga soo qaado in hoggaamiyayaal sare oo ka tirsan al-Shabaab ay weerarayeen Godane todobaadyadii lasoo dhaafay, sii deeynta warqaddu kadiso ma noqon, waliba gaar ahaan tan iyo markiifarriintiisii maqalka aheyd ee uu bishan bilowgeeda usoo diray taageerayaashiisa ay ku guul-darreysatay in ay ha hadasho khilaafka sii koraya ee ka dhex jira madaxda ururka.
Iyada oo ah Isku day lagu doonayo in la isku sii hayo xubnaha al-Shabaab, ayay warqaddu sii taraaraysaa illaa iyo ay gaarto heer ay soo xigato xadiis dhidibbada loogu adkeeynayo xilka hoggaamineed ee Godane.
"Haddii aad bayco la gashaan hoggaamiye, aadna siisaan aqoonsigiina, waa in aad addeecdaan inta aad awoodaan. Haddii nin kale uu u yimaado si uu ula dagaalamo hoogaamiyahan, gooya madaxa kan kale," ayuu leeyahay xadiiska lasoo xigtay.
Warqaddu waa ay sii socotay iyada oo ahayd isku day lagu doonayo in lagu dhaawaco hoggaamiyayaasha kale magacoodana lagu ceebeeyo.
"Dad juhalo ah ayaa bilaabay in ay ka hadlaan caqiidada ayna soo saaraan xukuno," ayaa warqadda lagu sheegay. "Fulayo ayaa bilaabay in ay ka hadlaan arimaha jihaadka, halka dad quuri-waayayaal ahna ay bilaabeen in ay dhalleeceeyaan hoggaamiyayaasha qaranka. Tani waxaaka dhashay in Islaamka la gaarsiiyo xanuun jaahilnimo, gaalnimo iyo nifaaq."
"Haddii aad jaha wareerto, weydii culimada iyo hoggaamiyayaasha mujaahidiinta, oo waano u raadso kuwa wax ka yaqaana taariikhda jihaadka," ayay warqaddu ku dartay, inkasta oo kuwa sida aadka ah u dhalleeceynaya Godane ay yihiin culimada iyo hoggaamiyayaasha Mujaahidiinta.

Warqadda oo ku andacooday in 'mareego qaar' ay xumeeynayaan muqaalka jihaadka

Warqadda ayaa sidoo kale sheegatay in hay'adaha warbaahinta ee gobolka ka jira ay marin-habaabinayaan xaqiiqda si ay u xumeeyaan sawirka Godane iyo sheegashadiisa ku aaddan "jihaadka dhabta ah".
"Halkan, waxaan ku caddaynaynaa in wararka laga sii daayay mareegaha qaar si loogu xumeeyo sawirka dhabta ah ee jihaadka ka jira Soomaaliya ay aad uga fogyihiin runta; waxaa ka buuxay been abuurasho, shakiyo iyo in macluumaadka loo adeegsado si aad uga duwan xaqiiqda," ayaa warqadda lagu sheegay. "Waxaa lagu saleeyay wax aan jirin, xaasidnimo, xaqiirnimo iyo iyagoo hadallada ka rogay xaqiiqda."
Warqadda ayaa ula jeedday mareegaha warbaahinta isa soo taraya ee gobolka oo hadda doonaya -- kadib sannado laga baqayay in si toos ah looga hadlo arrimaha al-Shabaab -- in ay daabacaan maqaallo lagu durayo ururka al-Qaacidda la jaalka ah, sida falanqeeyn lagu sameeyay warqado xiriir ahaa oo ay qoreen hoggaamiyayaasha al-Shabaab ee kasoo horjeeda hoggaaminta Godane.
Tusaale ahaan, 6-dii Abriil, ninka wax ka aasaasay al-Shabaab Ibrahim al-Afghan ayaa warqad furan u diray hoggaamiyaha al-Qaacidda Ayman al-Zawahiri taa oo si weyn u dhaleeceysay Godane isagoo al-Qaacidda ka dalbaday in ay soo faragaliso si ay al-Shabaab uga badbaadiso "godka mugdiga ah". Al-Afghan, oo magaciisa dhabta ah uu yahay Ibrahim Xaaji Jaamac Meecaad, oo sidoo kale loo yaqaano Abu Bakr al-Zaylici, ayaa warqaddiisa ku faahfaahiya sida Godane uu u noqday kaligii taliye, isagoo abuuraya jawi ka maran fikrado cusub, qof walba oo su'aal weydiiyana ku tilmaama khaa'in.
Labo todobaad kadib, hoggaamiye sare oo al-Shabaab ka tirsan oo la jaal ah dagaalyahanada shisheeye, al-Zubayr al-Muhajir, ayaa isaguna warqaddiisa furan ku baahiyay internetka, isagoo taageeray farriinta al-Afghan, kuna faahfaahiyay sida Godane uu u cayriyay dagaalyahanada shisheeye ee Soomaaliya jooga, isagoo kula dhaqmaya si ixtiraam darro ah.
Isagoo xaaladda kusii xumeeyay Godane, ayuu Omar Hammami, jihaadiga Mareykanka u dhashay ee loo yaqaano Abu Mansour al-Amriki, ku eedeeyay taageerayaasha Godane in ay isku dayeen in ay dilaan bishii hore.
Iyagoo taa ka jawaabayay, ayay al-Afghani, al-Muhajir, iyo hoggaamiyaha sare ee al-Shabaab Sheekh Mukhtaar Roobow Cali iyo, hoggaamiyaha Xisbul Islam Sheekh Xasan Daahir Aweys waxay 30-kii Abriil si wadajir ah u faafiyeen fatwo ay ku xaarantimeeynayaan dilka al-Amriki.
Haddii wararka aan la xiqiijin ee tilmaamaya in dagaalyahanno daacad u ah Godane ay dileen al-Amriki 7-dii Maajo ay run yihiin, waxa ay taa caddeyn u tahay iska indha tiridda Godane ee fikradaha diineed iyo arrimaha kale, ee ka imanaya hoggaamiyayaasha al-Shabaab ee fatwadan soo saaray.
Su'aal: Ilaa intee ayaad u malaynaysaa in Godane uu sii ahaan doono hoggaamiyaha ugu sareeya ee al-Shabaab iyadoo kala qeybsanaantan ay jirto? Fadlan fikraddaada la wadaag santuukha fikradaha ee hoos ku yaalla.

0 comments:

Post a Comment