ABDULKARIM SUMA





Thursday, October 31, 2013

Mama Yangu!! Uvumilivu wamshinda Irene Uwoya! Alichokiandika hapa watoto chini ya miaka 18 msisome!


Mama Yangu!!  Uvumilivu wamshinda Irene Uwoya! Alichokiandika hapa watoto chini ya miaka 18 msisome!

    “...Wale ma-(Tusi linalohusisha kiungo cha mwili) wanao post (Tusi kama la hapo mwanzo) humu...waaandike watakavyo...sio (Tusi- vitendo vibaya kwenye jamii) tuuu yan na vza yakuzunguka dunia nzima....siitaj watu ma-(Tusi kali sana)...kama na kuboa kafe mbele....eti range nimehongwa mtasubiri sanaaaa....sina mdaa huo sinaaa...wakukaa pemben na kumsmanga mtuuuu...wote mnao ni disss ma-(Tusi la kumalizia sentensi)...
    Hayo ni maneno ya mwadada Irene Uwoya aliyoaandika usiku wa leo hii kupitia ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii. Tulipoyasoma tuu, tulishtushwa sana kwani si kawaida kwa mwanadada huyu kuandika maneno mzito kama haya na ndipo tulipoamua kufanya utafiti yakinifu ili tujue why??? Na haya ndo majibu ya uchunguzi wetu huu…
    Tujikumbushe Historia fupi
    Hivi majuzi mwadada Irene Uwoya alipost kwenye mtandao picha za gari yake mpya aina ya Range Rover na ndipo watu wengi walianza ku-comment na “kumponda” mwanadada huyu kuwa sio yake bali kahongwa na wanaume “wanaomuweka mjini”
    Irene akajibu
    Siku si nyingi baadae Irene aliwajibu kwa kusema kuwa gari hiyo ni yake na wote wanaosema kahongwa watasubiri sana maana hiyo ni matokeo ya jasho lake
    Msiba wa baba yake wema wahusishwa
    Kwa bahati mbaya mwanadada Wema Sepetu alipata matatizo ya kufiwa na baba yakehivi majuzi na ndipo zikatoka tetesi kuwa ETI mwanadada Irene pamoja na kundi jingine la mastaa Fulani wamesusa kuhudhuria msiba huo kwa madai kuwa Wema huwa hashiriki misiba ya wengine
    Mashabiki wa wema wamjia juu
    Baada ya mambo hayo yote hapo juu ndipo kundi la mashabiki wa wema walipoanza kuandika kwenye ukurasa wa mwanadada huyo, wakimutukana na kumponda sana eti hilo gari sio lake bali kahongwa na jamaa mmoja hivi (Jina tunalihifadhi kwa sababu za kiusalama) na hivyo asiwadanganye wananchi mambo ambayo si kweli
    Uvumilivu ukawa mchache kwa Irene
    Baada ya matusi na maneno mengi ya kejeli toka kwa mashabiki hao kumzidi Irene hatimaye ndio ameamua kuandika hayo hapo unayoyaona juu. Daah, hatari sana mjini hapa ukiwa staa.

    0 comments:

    Post a Comment