ABDULKARIM SUMA





Sunday, October 13, 2013

MWANDISHI WA ITV UFOO SARO AHAMISHIWA ICU BAADA YA KUJERUHIWA KWA RISASI

Mwandishi wa habari wa ITV/Radio One Ufoo Saro amejeruhiwa kwa risasi na mtu anaedaiwa kuwa ni mchumba wake na pia mtu huyo kumpiga risasi mama mzazi wa Ufoo na kisha yeye mwenyewekujipiga risasi  na kufariki dunia papo hapo leo alfajiri eneo la kibamba jijini Dar esSalaam 

Awali taarifa zilizosikika katika vyombo vya habari vya ipp ambapo Ufoo anafanyia kazi  zilisema kuwa Mwandishi wa habari wa Kituo Cha Habari cha ITV na Radio One UFO SARO amepigwa risasi mbili na anayesemekana kuwa ni Mchumba Wake aliyekuwa akifanya Kazi Sudan Kupitia UN.

  Sababu ya Kupigwa Risasi yeye UFO SARO na Mama yake Mzazi Ufo Saro ambaye amepoteza maisha papo hapo ni ugomvi ambao haujajulikana na huku Aliyewapiga risasi UFO SARO pamoja na Mama yake Mzazi Ufo kajipiga risasi chini ya kidevu na kupoteza maisha papo hapo..

Habari zilizotufikia hivi sasa zinasema Ufoo kwa sasa amehamishiwa katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) Kwa uangalizi zaidi.

tuendelee kumuombea ili apate unafuu na arejee katika kazi zake za kila siku za kuhabarisha umma.tutaendelea kuwahabarisha zaidi kwa kadri tutakavyokuwa tunapata taarifa kuhusu hali yake.

0 comments:

Post a Comment