Staa wa ‘number one’ Diamond Platnumz leo December 25 2013 ameiweka bongofleva kwenye headlines za kipekee ambazo ni chache kutokea baada ya kuwatangaza watoto watatu ambao amejitolea
kuwasomesha kutokana na kushinda kwenye shindano lake la kumtafuta anaejua kucheza ‘ngololo’ ndani ya Christmas.
kuwasomesha kutokana na kushinda kwenye shindano lake la kumtafuta anaejua kucheza ‘ngololo’ ndani ya Christmas.
Party ilifanyika Leaders Club Kinondoni 88.5 Dar es salaam na kuhusisha pia michezo mbalimbali kama kukimbia, kucheza mpira na vingine kibao.
Hawa watoto watatu unaowaona hapa kwenye hii picha juu wawili wa kiume ndio walishinda kwa kucheza sana na mmoja wa kike Diamond alimpa nafasi ya upendeleo kwa sababu hakupatikana mshindi wa kike hivyo akasema atagharamia elimu yake ya Sekondari.
Namkariri Diamond akisema ‘bongofleva’ ndio itawasomesha kwa kuwalipia ada za madarasa waliyobakiza kama ahadi inavyosema ni kwenye shule binafsi zenye viwango vikubwa kielimu.
Diamond anasema ‘hawa wawili walieko darasa la nne nitahakikisha Ngololo inawasomesha mpaka wamalize darasa la saba, tupige makofi mengi kwa miziki yetu kwa kufanya vitu hivi.. kwanza nawapa hizi zawadi ndogo, Management yangu imeniambia sio tu kuwalipia ada bali tutawahamishia kwenye shule za kimataifa zenye elimu nzuri zaidi, kesho na keshokutwa waje kuwa hata Marais wetu wathamini muziki wetu’
0 comments:
Post a Comment