ABDULKARIM SUMA





Wednesday, December 25, 2013

Kijana mmoja ashambuliwa hadi kufariki dunia baada ya kusemekana kwamba ni mchawi aliyedondoka na ungo

15
Wananchi wakiwa hasira kali wamempiga  hadi kumuua mwanaume aliyedhaniwa kuwa ni mchawi baada ya kuanguka akiwa amepanda ungo maeneo ya Mbezi Luis jijini Dar es Salaam.
Jamaa huyo mkazi wa Mwanza anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 20 hadi 25, alianguka jana saa 12 asubuhi maeneo ya Mbezi Luis baada ya kudai kuwa alikuwa kwenye safari zake za kishirikina.
Mashuhuda wanasema kabla ya kufariki alisema “Mimi nilikuwa na wenzangu sita, wanaume watatu na wanawake watatu ambapo tulikuwa tunatoka Mwanza kuelekea kwenye mkutano wetu”
“Lakini mimi kwa bahati mbaya nilikiuka masharti tuliyopewa na mkuu kwa kufungua macho ndipo ghafla nilianguka na kupata kadhia hii inayopelekea mauti yangu”
Hata hivyo kutokana na vurugu zilizokuwapo eneo hilo la tukio, ambapo wananchi wa eneo hilo walikuwa wanataka kumuua, kijana huyo alishindwa hata kutaja jina lake kutokana na kipigo alichokuwa anakipata kutoka kwao
16
17
19
20

0 comments:

Post a Comment