ABDULKARIM SUMA





Thursday, January 30, 2014

DAVINA: KULEA KUMENIKOSESHA DILI

STAA wa Bongo Movie, Halima Yahaya ‘Davina’ amefunguka kuwa mwaka 2013 aliutumia zaidi kwa kulea mimba hadi kujifungua hivyo kukosa madili ya kazi za uigizaji.

Akizungumza na paparazi wetu, Davina alisema mwaka huu amejipanga kurejea upya katika sanaa kwani amegundua kuwa mashabiki wake walikuwa wamemmisi hivyo lazima apambane kutetea taito yake katika sanaa.
“Nimejipanga zaidi mwaka huu, nimedhamiria kufanya mapinduzi makubwa katika sanaa tofauti na kipindi cha nyuma, kulea siyo mchezo ilibidi sanaa ikae pembeni kidogo,” alisema Davina ambaye sasa ni mama wa mtoto mmoja, Fazal.

0 comments:

Post a Comment