ABDULKARIM SUMA





Thursday, February 6, 2014

Unatoa alama ‘max’ ngapi kwa Kitale na Director wa movie hii juu ya hizi picha mbili.

1800193_628575777208218_1426278056_nMaigizo mengi sana nchini huwa yanalalamikiwa kukosa uhalisia wa tukio,hebu tumia dakika zako chache kuangalia namna picha hizi zilivyochanganywa ambazo zinamuonyesha Kitale kama kamkata kichwa huyo jamaa.

Kwa haraka haraka unaweza kudhani kweli lakini bado sijajua jina la movie hii ingawa kwa kisehemu hiki kinaonyesha kama ni movie inayoongea na vitendo zaidi,lakini najiuliza hapa mbona kichwa hakionekani maana kwa picha hii inaonekana kama jamaa ndo kamkata Kichwa muda huo.
Inawezekana labda hakikutakiwa kuwepo kwa mujibu wa muongozaji ‘Director’ .kwenye post za kitale picha ya juu aliipa maelezo’Jela kwetu si Disco’ na hii picha ya chini kaipa maelezo ‘Ukizingua tunazingua’ jina la movie hii bado hajaweka wazi ingawa wako kwenye hatua za utengenezaji.
1452246_628574977208298_346072955_n

0 comments:

Post a Comment