ABDULKARIM SUMA





Wednesday, February 12, 2014

Wale wa Director Nisher hii inawahusu.

nishaaUkizungumza jina la Director Nisher sasa hivi kwa mdau yoyote wa muziki anaweza asione kama jina geni kwake na hii ni baada ya kuingia rasmi kwenye sekta ya
uongozaji[Director]wa video mbali mbali za Bongo Fleva.
Miongoni mwa video alizozifanya ambazo imetoka taarifa kuwa zimepata ruhusa kuonyeshwa kwenye kituo cha Chanel O ni pamoja na Video ya Mirror ’My Baby’,Young Dee,Kijukuu’,G nako ‘Mama Yeyoo’ na video mpya ya Nikki wa pili ‘Nje ya Box’.
Nisher ambaye kabla hajaanza kuwa Director wa Video amewahi kuimba ingawa hakupata nafasi kubwa ya Watanzania kumuelewa kama walivyompokea kwenye Uongozaji wa Video Kiasili Nisher ni mwenyeji wa 87.9 Arusha.
nishaKupitia ukurasa wake wa Instagram Nisher ame-amplify taarifa hizi huku chini ya picha hizo akiandika maneno yafuatayo>“Video zingine kuanza kuoneshwa Channel O ni pamoja na “Baby” Ya Mirror, “KIJUKUU”, ya Young Dee, na “MAMA YEYOO” Ya G.nako….All these videos Directed by NISHER! Namshukuru Mungu!”
Screenshot_2014-02-12-10-19-43
Nisher ambaye anasema imemgharimu Miaka 12 Kujua Mambo Ya Video Directing/Films/Television/Acting na Commercials Na bado anajifunza.

0 comments:

Post a Comment